Wednesday, February 20, 2013

Wanenavyo kuhusu Matokeo From IV

Div 1 - 1,641
Div 2 - 6,453
Div 3 - 15,426
Div 4 - 103,327
Div 0 - 240,903



Mimi binafsi siyakubali. Jibu liko kwa walimu. Serikali igeuke nyuma iwatazame walimu, si kwa kutumia polisi, usalama na kuwakata mishahara, bali kwa matendo mema – mishahara mizuri, marupurupu sahihi na kwa wakati, motisha, kuwapandisha vyeo kwa wakati, kuwalipa gharama za uhamisho. Upande wa pili na kuongeza walimu, madarasa, madawati, vitabu na vifaa nyingine muhimu. Baada ya hapo, ni haki na wajibu, kazi na dawa, asiyefanya kazi na asile, asiyefaulisha abanwe.
Wadau wa elimu wanena:

Imagine the future of a country that fails 84% of her young population.

Form 4 results out, 60% (240,903) fail! It's NATIONAL DISASTER ! It's emergency! Urgent serious steps must be taken NOW.

Disastrous Form 4 Results. Div 1 - 1,641; Div 2 - 6,453; Div 3 - 15,426; Div 4 - 103,327; Div 0 - 240,903. Div 1-3: Boys 16,342, Girls 7,178

Mwaka jana tumelalamika, tukasahau. SASA tufanye kitu. Waziri wa Elimu atoke. Wizara iwe chini ya Rais. Yakiwa haya mwakani, na yeye atoke
Kucheza na Elimu tutaula wa chuya kwa uvivun wa kuchagua. Miradi yote tufanyayo, bila Elimu bora ni UPUUZI tu. Elimu BORA na BURE
Hawa watoto waliopata zero na four haraka sana wapate mafunzo ya ufundi. VETA kila Wilaya ni ya lazima SASA
Halafu Wizara ya Elimu iwe chini ya Ofisi ya Rais. Mwakani wakifeli kama hivi na yeye atoke.............. tufanye petition
Naenda kulala sasa. Haya matokeo ya kidato cha nne haya bila hatua ya uwajibikaji kufanyika....... Kawambwa has to go! Hakuna namna kabisa

Still no breaking news "Waziri wa Elimu ajiuzuru" kweli TZ noma kweli kweli hamna uajibishwaji wala kujiajibisha.









No comments:

Post a Comment