Thursday, March 13, 2008

Mwananchi Queen

Hiki ndio Kikosi Kamili cha makwini wa Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd, inayochapisha magazeti ya Mwananchi, mwanaspoti, Mwananchi Jumapili, The Citizen na Sunday Citizen. Kikosi hiki kikiongozwa na mama lao, Maimuna Kubegeya (Mbele Kushoto) kimefanikiwa kwa mbinde kuingia fainali ya Mashindano ya NSSF

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 6:52:00 PM | Permalink | Weka Maoni 2

Tuesday, March 11, 2008

Makaburi mengine balaa

Kaburi kwa sura ya gari. Hii ni zawadi ya Marehemu Joely Kivelege aliyezikwa Kinondoni Dar es Sa Salaam, aliyopewa na Mzungu mmoja aliyekuwa mlezi wa kituo cha watoto yatima. Kivelege alikuwa miongoni mwa watoto hao. Mzungu huyo alimpenda sana kutokana na tabia yake njema. Alipotaka kwenda Ulaya likizo, alimuahidi kijana huyo zawadi ya gari, lakini aliporudi, alikuta mambo yameharibika. Kivelege alikuwa amefariki kwa malaria iliyopanda kichwani. Ahadi ni deni, mzungu huyo aliamua kumjengea kaburi mfano wa gari na hiyo ikawa ndiyo zawadi yake.

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 2:03:00 PM | Permalink | Weka Maoni 2

Tuesday, March 04, 2008

Kila mtu na 'Ushujaa' Wake

Waziri Mkuu, Mizengi Kayanza Peter Pinda akikabidhiwa upinde na mishale ili akapambane. Waziri Mkuu aliyestaafishwa, Edward Ngoyai Lowassa akionyesha ngao yake ya kujikinga dhidi ya mishale

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 1:38:00 PM | Permalink | Weka Maoni 3

Monday, March 03, 2008

Mafisadi Wazidi Kubanwa

Wanafunzi wa vyuo mbalimbali vya Mbeya, Tanzania wakionyesha bango lenye katuni inayomuonyesha kiongozi mmoja, wakimuuliza; fedha zote hizi unazipeleka wapi? Bila nao wamekerwa na wizi wa mapesa ya umma.

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 12:13:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Cheka Awacheka Kina Matumla

Taarifa kutoka katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Bondia Froncis Cheka wa Morogoro amemchakazi vibaya Hassan Matumla kwa KO na kutwaa ubungwa wa mabara uzito wa kati. Alimuangusha katika round ya 10 kati ya 12 zilizotakiwa. Kwa hiyo Cheka ameendelea kucheka katika familia ya wanamasumbwi ya kina matumla, baada ya kuwachapa hata kakaze Hassan.

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 12:03:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Friday, February 29, 2008

Ndondi Ndondi

Hassan Matumla (kulia) na Hassan Cheka wakitunishiana misuli wakati wa kutangaza mtanange wao wa kesho ili kuwania mkanda huu.

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 7:25:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Waliyokubaliana, Kibaki na Raila

Key points: Kenya power-sharing deal

  • The post of prime minister will be created, with the holder having the authority to co-ordinate and supervise the execution of government functions.

  • The prime minister will be an elected member of parliament and the parliamentary leader of the largest party in the National Assembly, or of a coalition if the largest party does not command a majority in parliament.

  • Two deputy prime ministers to be appointed, one to be nominated by each member of the coalition.

  • The prime minister and deputy prime ministers can only be removed if the National Assembly passes a motion of no-confidence with a majority vote.

  • A cabinet to consist of a president, vice-president, prime minister, two deputy prime ministers and other ministers. The removal of a minister of the coalition will be subject to consultation and agreement in writing by the leaders.

  • The composition of the coalition government will at all times take into account the principle of portfolio balance, and reflect the parties' relative parliamentary strengths.

  • The coalition will be dissolved if the current parliament is dissolved; or if the parties agree in writing; or if one coalition partner withdraws from the coalition.

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 2:08:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Chemical Ali naye Kunyongwa

Bila shaka, kwa waliofuatilia vita ya Iraq, mnamkumbuka mjombawe Saddam Hussein, Chemical Ali...Naye amehukumiwa kunyongwa hadi kufa. Taarifa yenyewe iko hivi.
BAGHDAD - Iraq's presidency endorsed the execution of Saddam Hussein's cousin known as "Chemical Ali," who was sentenced to death for his role in the 1980s scorched-earth campaign against Kurds, a government adviser said Friday. The backing by Iraq's President Jalal Talabani and two vice presidents is the final step for the approval of Ali Hassan al-Majid's death sentence, which must be carried out within 30 days of the decision.

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 12:29:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Kenya Waafikiana. Amani Kurejea?

Wazee wa kazi wakubaliana kugawana madaraka

Hapa Watiliana saini, tuone nani atakuwa wa kwanza kukiuka makubaliano

Hata 'wazee' wetu walioshindwa miafaka kibao ya Zanzibar, walikuwepo, labda wamepata somo

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 11:33:00 AM | Permalink | Weka Maoni 0

Tuesday, February 26, 2008

Juhudi za Mbowe Hola!

Pamoja na Ushawisho wooote wa Mwenyekiti wa Chadema kumnadi mgombe wake, Victor Kimesera bado kapoteza. Unamuona mfanyabiashara Kimesera anavyofurahia, akidhania ataibuka mbunge baada ya kushindwa mara tatu jimboni humo. Kumbe sasakapoteza mara ya nne.

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 10:15:00 AM | Permalink | Weka Maoni 0

Wapinzani Wavyopoteza Kiteto

WanaCCM wakishangilai ushindio wa Benedict ole Nangaro kuwa Mbunge wa Kiteto

Mwanzoni Chadema walishani mgombea wao, Victor Kimesera ndio ameshinda baada ya kuona matokeo ya mjini Kibaya, lakini kumbe, mambo yakawa kama Kenya...Kibaki (Nangaro) kaitangazwa mshindi Odinga (Kimesera) Mhh!.

FFU walikuwa kibao. Taarifa zilisema walikuwa zaidi ya 500. wote wilaya moja, kufanya kazi gani? au walikuwa wanapiga kura?

Kapteni John Komba wa TOT na Mbunge wa Mbinga Magharibi akishuka kkwenye chopa ambayo ilitumika kama silaha ya msaada baada ya Bendi yake kushindwa kufua dafu kuwashawishi watu wa Kiteto

Wapiga kura wakiangalia majina yao kwenye daftari (karatasi) za kudumu za wapiga kura. Inasemekana zaidi ya nusu ya wapiga kura hawakuona majina yao. Wengine yalikuwa kwenye vituo vya mbali na walipotarajia...Baadhi sijui wa chama gani walihamishwa kwa magari kwenda kupiga kura mbali majina yao yalipopelekwa.

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 10:02:00 AM | Permalink | Weka Maoni 0

Vita ya Chopa

CCM YATANGAZWA MSHINDI KITETO CCM kwa muda mrefu ilikuwa inasema matumizi ya helkopta ni matumizi mabaya ya fedha kwa Chadema. Ilipoona inakabwa koo, nayo ikakodi chopa hii, sababu ya matumizi ikaisha, wakasingizia hali ya hewa. Siku chopa yao ilipoanza kazi, ya Chadema 'ikafia' Dodoma. Hapo huenda ndipo mambo yakaharibika.

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 9:56:00 AM | Permalink | Weka Maoni 0

Muungwana husikiliza

Baadhi waliniandikia hapa, wengine wakaandika kwa email baada ya kushindwa kutoa maoni katika kisanduku cha maoni. Wengine walinipigia simu na wachache wakanieleza kwa mdomo. Nimeona sina sababu ya kuwa mkaidi...Nimerudi.

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 9:43:00 AM | Permalink | Weka Maoni 2

Monday, February 18, 2008

KWAHERINI

Ndugu wasomaji wa Blog hii
Kwaherini. Ninawaaga nimeamua kuachana na blog. Asanteni kwa kuniunga mkono tangu Novemba 2006.
Ndimi Miruko

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 5:41:00 PM | Permalink | Weka Maoni 9

Joji Bush kwenye Benchi la Wagonjwa

Mzee wa Vituko: Bush kwenye benchi la wagonjwa Arusha Mzee unamshika kila mtu, angalia usirudi US na 'Nairobi Red Eyes'

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 4:44:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

JK akinga bakuri; Bush amwaga vyandarua

Jana mjini Arusha Rais Kikwete alielelzea tatizo la malaria nchini kwa Bush, naye hakuwa na ajizi...Endelea. PRESIDENT KIKWETE: Mr. President, today there are thousands of women and children who would have died from malaria that are alive in Tanzania and all over the country, thanks to your malaria support program. I can give the example of Zanzibar. In 2004, in the outpatient clinic, 500,000 malaria patients were treated; in 2007, only 10,000. (Applause) In 2004 in Zanzibar, 40 percent of the patients tested positive for malaria; in 2007, only 5 percent. (Applause.) When the blood slide is taken, 35 percent tested positive for malaria in 2004; in 2007, only 1 percent. (Applause.). PRESIDENT BUSH: Today, I'm pleased to announce new steps in the bed net campaign. Within the next six months, the United States and Tanzania, in partnership with the World Bank and the Global Fund, will begin distributing 5.2 million free bed nets. This ambitious nationwide program will provide enough nets to protect every child between the ages of one and five in Tanzania

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 3:50:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Bush Alipotembelea A-Town

Joji Kichaka akutana na akinamama wa Kimasai, KIA, huku mkewe, Laura akiwatazama kwa mshangao

Baada aya Kilio cha Malaria kutoka kwa JK, Bush aalitoa vyandarua milioni 5 kuwasaidia wabongo wasife kwa mbu. Baba ana huruma huyu!

Mama akazawadiwa chandarua na mzee Bush kufaidi joto lake. Walau si haba.

Labels:

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 3:35:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Bush

George Bush akicheki Ngoma Ikulu ya JK Bush akiwapa mkono wachezaji wa ngoma

Shein akiwa ameketi na Mke wa Bush, Laura wakati wa chakula cha usiku

Kikwete na Makamu wake, Dk Shein, wakigonganisha glasi na wageni wao Ikulu

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 1:27:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Sunday, February 17, 2008

Bush in Africa

Kiatu cha Bush Kicheko cha Bush Kumbe anapenda mademu

Makachero wa Bush wanoko kama wako kwao!

Hawana imani na Ikulu ya JK, Yaani hadi kwenye paa

Labels:

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 4:38:00 PM | Permalink | Weka Maoni 1

Saturday, February 16, 2008

BUSH IN TZ

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 10:31:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Mtoto adondoka kutoka kwenye 'ndege', apona

Mtoto huyu (katikati) akiwa katika Ofisi za Mwananchi, akisimulia kisa chake. Kushoto ni mwandishi wa Mwananchi na Kulia na Padri wa Parokia ya Kristo Mfalme, Tabata aliyemsindikiza. KISA KAMILI:
Na Peter Edson MTOTO mwenye umri wa miaka 12 mkazi wa kijiji cha Kilima Hewa mkoani Mtwara amekutwa akiwa uchi kwenye eneo la Kanisa la Kristo Mfalme, Tabata jijini Dar es salaam baada ya kuanguka kutoka kwenye ungo waliokuwa wakisafiria kishirikina. Akiongea na Mwananchi Jumapili, mtoto huyo alisema yeye na bibi yake, Binti Abdala Mkumba walikuwa wakisafiri kutoka Mtwara kwa usafiri wa ungo wakielekea mjini Morogoro kwenye mkutano wa wachawi wapatao 50 wenye lengo la kumpokea mwenzao aliyejiunga katika kundi lao hivi karibuni ili kumjengea nguvu na uwezo wa kupambana na nguvu nyingine zaidi soma www.mwananchi.co.tz

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 7:07:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Ukitaka kwenda Makete hivi sasa inahitaji moyo Angepelekwa Bush ili aone, au? Basi hili linaweza kumaliza hata wiki mbili bila kuvuka hapa...Tanzania yetu na mafisadi mh!

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 6:00:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Kichaka Aingia Afrika

Bush akiwa na Rais wa Benin, Thomas Boni Yayi Hapa Joji Kichaka akimbusu mkewe, Laura, baada aya kutunikiwa medali ya heshima ya Benin Akiwa na Rais kwenye zuria jekundu. Hivi nani alipanga mazuria hayo kuwa mekundu duniani pote? Nyuna inaonekana Air Force One Akikagua jeshi la Benin

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 4:27:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Friday, February 15, 2008

Karibu Rais Bush

Page 3

Labels:

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 3:05:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Thursday, February 14, 2008

Diallo Akisoma Gazeti Bungeni

Aliyekuwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo, Antony Diallo (kulia), akijipatia habari katika gazeti la Mwanahalisi, lililokuwa na headline: Richmond ya Rostam -Ikulu. Anayesikiliza mjadala wa bunge ni Mbunge wa Pangani, Mohamed Rished

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 12:44:00 PM | Permalink | Weka Maoni 1

Wednesday, February 13, 2008

Wazushi Wameshaanza Mambo Yao

Labels:

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 5:42:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Kazi kwao Celtel

Kazi kubwa iko kwa wateja wa Celtel kuongea kwa wingi kushindani haya ma-RAV4 na LandCruiser moja.

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 5:03:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Mawaziri Waapishwa Dodoma

Kilichovutia wakati wa hafla ya akuapishwa kwa mawaziri ni watu wengi katika viwanja vya Ikulu ndogo , Chamwino Dodoma, kuimba Tyson, Tyson, Tyson, mara baada ya kuapishwa Stephen Wasira, Waziri pekee muda mrefu ambaye alikuwa serikalini tangu Awamu ya Kwanza. Sasa amekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Aliwahi kuhamia upinzani, NCCR-Mageuzi na kuwa mbunge.

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 2:08:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Baraza la Mawaziri

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 9:24:00 AM | Permalink | Weka Maoni 0

Tuesday, February 12, 2008

Mawaziri 17 Wapoteza

* Wamo mawaziri kamili 9, manaibu 7 * Baadhi yao waliomba kupumzika Mawaziri waliokumbwa na 'panga' hilo 1. Zakhia Meghji (Fedha) 2. Anthony Diallo (Maendeleo ya Mifugo) 3. Basili Mramba (Viwanda, Biashara na Masoko). 4. Joseph Mungai (Mambo ya Ndani) 5. Dk Juma Ngasongwa (Mipango, Uchumi na Uwezeshaji) 6. Kingunge Ngombale-Mwiru (Ofisi ya Rais-Siasa na Uhusiano na Jamii) 7. Dk Ibrahim Msabaha (Ushirikiano wa Afrika Mashariki) 8. Nazir Karamagi (Nishati na Madini). 9. Juma Mwapachu (Usalama wa Raia) Manaibu mawaziri waliochwa ni 1. Abdissalaam Issa Khatib (Fedha) 2. Ludovick Mwananzila (Elimu na Mafunzo ya Ufundi). 3. Daniel Nsanzugwanko (Habari, Utamaduni na Michezo) 4. Dk Charles Mlingwa (Maendeleo ya Mifugo) na Gaudence Kayombo (Mipango, Uchumi na Uwezeshaji). 5. Ritha Mlaki (Aridhi na Maendeleo ya makazi) 6. Gaudence Kayombo (Mipango, Uchumi na Uwezeshaji) 7. Dk Luka Siyame (Ofisi ya Waziri Mkuu-Maafa)

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 7:27:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Mawaziri 'wapya' Kuapishwa kesho Mchana

Taarifa ya Ikulu: Baraza Jipya la Mawaziri litaapishwa na Rais Jakaya Kikwete (pichani) kesho Jumatano saa 7.30 mchana Ikulu ndogo ya Chamwino, Dodoma. Idara ya Mawasiliano Ikulu Februari 12

Labels:

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 6:37:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Baraza Dogo, Sura Chache Mpya

1. WAZIRI OFISI YA RAIS (UTAWALA BORA) SOFIA SIMBA 2. WAZIRI OFISI YA RAIS (MENEJIMENTI YA UMMA) HAWA GHASIA 3. WIZARA OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO) MOHAMED SEIF KHATIB 4. WIZARA YA UTALII NA MAZINGIRA DK. BATILDA BURIANI 5. WAZIRI OFISI YA MAKAMU WA RAIS (SERA NA URATIBU WA BUNGE), PHILIP MARMO 6. WIZARA YA TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, STEVEN WASIRA 7. WIZARA YA FEDHA MUSTAFA MKURO NA MANAIBU NI JEREMIAH SUMARI NA OMARI YUSUF MZEE 8. WIZARA YA AFYA PROFESA DAVID MWAKYUSA NAIBU NI AISHA KIGODA 9. WIZARA YA ARDHI JOHN CHILIGATI 10. ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI PROFESA JUMANNE MAGHEMBE MANAIBU GAUDENSIA KABAKA NA MWANTUMU MAHIZA 11. WIZARA YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA DK SHUKURU KAWAMBA NAIBU NI DK. MAUA DAFTARI 12. WIZARA YA MIUNDO MBINU ANDREW CHENGE NAIBU DK. MAKONGORO MAHANGA 14. WIZARA YA UTAMADUNI NA MICHEZO GEORGE MKUCHIKA, NAIBU JOEL BENDERA 15. WIZARA YA KAZI NA AJIRA POFESA JUMA KAPUYA NAIBU HEZEKIA CHIBULUNJE 16. WIZARA YA MAJI PROFESA MARK MWANDOSYA NAIBU CHIZA 17. WIZARA YA KILIMO NA CHAKULA MATHAYO DAVID MATHAYO 18. WIZARA YA MENDELO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MARGARETH SITTA NAIBU NI DK LUCY NKYA 19. WIZARA YA UVUVI NA MIFUGO JOHN POMBE MAGHUFULI NA MANAIBU NI SHAMSA MWANGUGA NA EZEKIEL MAIGE 20. WIZARA YA MAMBO YA NDANI LAWRENCE MASHA NAIBU NI HAMISI KAGASHEKI 21. WIZARA YA MAMBO YA NJE NI BERNARD MEMBE, NAIBU SEIF ALI IDDI 22. WIZARA YA NISHATI NA MADINI WILLIAM NGELEJA, NAIBU ADAM MALIMA 23. WIZARA YA SHERIA MATHIAS CHIKAWE 24. WIZARA YA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA DK. HUSSEIN MWINYI NAIBU DK EMMANUEL NCHIMBI 25. WIZARA YA AFRIKA MASHARIKI DK. EMMANUEL KAMALA 26. WIZARA YA VIWANDA NA BISHARA DK. MARY NAGU NAIBU CYRIL CHAMI

Labels:

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 5:58:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Huyu Dingi Vipi, Abaki au Aondoke?

Mzee Kingunge Ngombare-Mwiru anaonekana akiondoka. Ndio moja kwa moja au atarudi? Toa maoni yako

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 11:18:00 AM | Permalink | Weka Maoni 0

Zigo la Richmond

Hii ndiyo mitambo ya Richmond ikishushwa kutoka kwenye dege kubwa la mizigo kutoka Marekani mwaka jana. Balaa lote lilianzia hapa, kwani mzigo huu ndio pekee uliowezekana. Mwingine uliletwa na Kampuni ya Dowans baada ya Richmond kushindwa kabisa.

Labels:

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 11:10:00 AM | Permalink | Weka Maoni 0

Richmond Ilivyozua Mambo

Hawa waliokuwa mawaziri kabla ya kutemeshwa, Profesa Peter Msolla na Margaret Sitta wakiondoka kwa staili za kila aina. Je watarudi leo?

Labels:

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 11:00:00 AM | Permalink | Weka Maoni 0

Bara la JK Utata

Baraza la JK lapipigwa tena danadana. Taarifa kamili: PRESIDENT’S OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR ES SALAAM. Tanzania. TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Rais Jakaya Mrisho Kikwete anatarajia kutangaza Baraza la Mawaziri leo(12/02/2008) saa 9.00 alasiri katika ukumbi wa TAMISEMI, Dodoma, badala ya saa 4.00 asubuhi kama ilivyotangazwa awali. Wahariri/Waandishi/Wapiga picha wawe wamewasili ukumbini saa 8.00 Mchana na walewenye waandishi wao Dodoma wawaeleze vema ili wazingatie muda. Ahsante na karibuni. Kurugenzi ya Mawasiliano, Ikulu, Chamwino DODOMA. 12/02/2008 . Zipo tetesi za kuingiza wapinzani kutoka Chadema na CUF. Yawezekana kweli ni mpango wake, lakini inawezekana amevujisha makusudi ili kusikia wananchi wanasemaje.

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 10:51:00 AM | Permalink | Weka Maoni 0

Saturday, February 09, 2008

Pinda Aapishwa

Waziri Mkuu Mizengo Peter Kayanza Pinda tayari ameapishwa. Ameapa kuwa mtiifu kwa Rais, Katiba, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kutokutoa siri za baraza la mawaziri.

Labels:

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 12:56:00 PM | Permalink | Weka Maoni 1

Friday, February 08, 2008

Mawaziri Wakuu Tanzania

Redg copy JULIUS Kambarage Nyerere alipewa nafasi hiyo na wakoloni Septemba 2,1960 hadi Mei Mosi, 1961 alirejea wadhifa huo Mei Mosi, 1961 hadi Januari 22,1962. Rashidi Kawawa alishika wadhifa huo Januari 22, 1962 hadi Desemba 9,1962. Pia, aliteuliwa kuendelea na nafasi hiyo Februari 17, 1972 na Februari 13,1977. Edward Sokoine aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu Februari 13,1977 hadi Novemba 7, 1980 baada ya kwenda masomoni aliporejea aliteuliwa tena Februari 24, 1983 hadi Aprili 12, 1984 alipopata ajali akitokea Dodoma bungeni na kufariki dunia. Cleopa Msuya alishika nafasi hiyo baada ya Sokoine kwenda masomoni Novemba 7, 1980 hadi Februari 24,1983. Aliteuliwa tena kushika wadhifa huo kuanzia Desemba 7, 1994 hadi Novemba 28, 1995 badala ya John Malecela. Salim Ahmed Salim, aliteuliwa Aprili 24,1984 hadi Novemba 5, 1985. Joseph Warioba alishika wadhifa huo kati ya Novemba 5, 1985 hadi Novemba 9, 1990. John Malecela alishika nafasi hiyo Novemba 9, 1990 na Desemba 7, 1994 baada ya kulazimishwa kujiuzulu. Frederick Sumaye, ndiye Waziri Mkuu pekee aliyeshika na nafasi hiyo kwa miaka 10 mfululizo tangu Novemba 28, 1995 hadi Desemba 30, 2005. Edward Lowassa aliteuliwa Desemba 30, 2005 hadi Februari 7,2008 baada ya kujiuzulu kutokana na Kamati Teule ya Bunge iliyoundwa kuchunguza mchakato wa zabuni ya uzalishaji umeme wa dharura ulioipa ushindi Kampuni Richmond Development ya Houston, Texas, Marekani kumhusisha na kuingia taratibu za kuisaidia.

Labels:

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 7:10:00 PM | Permalink | Weka Maoni 2

Wawili Wamkataa Pinda

Wabunge wawili wamemktaa Waziri Mkuu. Amepata kura za ndiyo 279. Mbili zilikuwa za Hapana. Moja imeharibika. Jumla ya kura zilikuwa 282. Hivyo, amethibitishwa kwa asilimia 98.9

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 6:29:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Kambi Zote Namkubali Pinda

Wabunge wote waliochangia hoja ya uteuzi, Kiongozi wa Upinzani, Hamad Rashid Mohamed, Waziri Mkuu alitepita, Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, Spika wa Bunge la Afrika, Getrude Mongela, Mwenyekiti wa UWT, Anna Abdallah, Mbunge Kijana kuliko wote, Zitto Kabwe na Mbunge mzee kuliko wote, John Malecela wameunga mkono uteuzi wa Kikwete. wamesema Mizengo Pinga ni mzoefu na mwadilifu kiasi cha kutosha. Sasa Kura zinapigwa.

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 5:40:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Taarifa za Uhakika

JK amekubali ombi la kujiuzulu la Dk Edward Hosea (kulia), Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru kuanzia saa 6.00 mchana leo. Anayekaimu ofisi hiyo nyeti, ni aliyekuwa naibu wake, Lilian Mashaka. Takukuru imetajwa kwa kuwalinda watuhumiwa wa ufisadi katika kashfa ya Richmond. Katika Kashfa hiyo kiongozi aliyetajwa na hajajiuzulu hadi sasa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, ambaye bila shaka alibakia ili kukamilisha kazi ya Rais ya uteuzi wa Waziri Mkuu na taratibu za kutangazwa kwake; na pengine kuapishwa kwake.

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 5:31:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

MIZENGO PINDA WAZIRI MKUU

Rais Jakaya Kikwete amemteua Mizengo Peter Kayanza Pinda kuwa Waziri Mkuu. Pinda ambaye ni Mbunge wa Mpanda Mashariki na alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 1:17:00 PM | Permalink | Weka Maoni 0

Du! Eti Leo Hana Mvuto!

leo

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 9:22:00 AM | Permalink | Weka Maoni 0

SERIKALI IMEBAKI NA WATU WAWILI TU

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali imesalia na viongozi wawili tu. Jakaya Kikwete, Rais na Makamu wake, Dk Ali Mohamed Shein. Basi. Hawa wawili sio wabunge. Bunge limeshindwa kuendelea asubuhi leo bila upande wa serikali. Limesitishwa hadi saa 11.00 jioni. Tunatarajia muda huo Waziri Mkuu Mpya atangazwe. Endelea kusoma hapa.

Imeandikwa na:Reginald S. Miruko Saa 9:05:00 AM | Permalink | Weka Maoni 0