Tuesday, April 28, 2009

Tuombe Likamilike Rugambwa Azikwe

Sehemu ya Mbele ya Kanisa Kuu (Cathedral) la Katoliki Jimbo la Bukoba linaloendelea kufanyiwa ukarabati wa muda mreeeefuuuu!
Upande wa Mashariki wa Kanisa hilo: Ndani ya Kanisa hilo ndimo aliyekuwa Kardinali wa Kwanza wa Mwafrika, Laurean Rugambwa alitaka azikwe, lakini wakati wa kifo chake, Desemba 8, 1997 lilikuwa linafanyiwa ukarabati, hivyo wahusika wakaamua kuupumzisha mwili wake kwenye Kanisa jingine la Kashozi, lililopo Km 15 Kaskazini mwa mji wa Bukoba, hadi watakapomaliza ukarabati. Hadi hii leo ukarabati huo haujakamilika. Haijulikani itakuwa lini... Bila shaka linahitaji maombi ya sala na misaada.

No comments:

Post a Comment