Wednesday, April 29, 2009

Tahadhari Kali Zaidi


Wakubwa, hadi sasa kuna taarifa mtandaoni kuwa watu kumi wameshapoteza maisha kwamshitukon na nyumba kadhaa zinaendelea kulipuka kwa mabomu kwaniyanaangukia kwenye mapaa ya nyumba hizo. Watu wote wanashauri kutokakabisa maeneo hayo.

Lakini Kamanda Kova kathibitisha vifo vya watu wawili tu. Jamani hali ni mbaya sana Mbagala yote nyeupe watu wamekimbia kabisa makazi yao. Waziri wa Ulinzi amedai kuna uwezekano wa mabomu mengine kuendeleakulipuka na kuleta madhara makubwa zaidi. Wameambieni watanzaniawenzetu waliohuko kama bado wapo wasikaribie maeneo hayo kabisa.

Pia, kuna mtu amenasa mawasiliano ya polisi wakielekezana kuwaeleza wafanyakazi walioko kwenye maghorofa jijini kurejea makwao, kwani mambomu makubwa zaidi (kama haya kwenye picha) yakilipuka inaweza kuwa kizaazaa. Magari Kibao ya jeshi yameelekea Mbagala.


Naendelea kufuatilia...

No comments:

Post a Comment