Wednesday, April 29, 2009

Milipuko ya Mabomu Dar. Duh!




Breaking News...
Huko Mbagala jijini Dar es Salaam ni kimuhemuhe, inasemekana ghala la silaha limeteketea kwenye kambi ya jeshi na mambomu kutikisa jiji zima. Habari zilizotufikia, zikakaririwa na Mzee wa Mshitu aliyeko kwenye chungu cha news, zinasema kuwa nyumba kadhaa zimeungua moto, mtu mmoja kufa na wengine kibao kujeruhiwa kutokana na mlipuko mkubwa wa mabomu umetokea katika jiji la Dar es salaam katika eneo la jeshi Mbagala Kizuiani.

Kwenye mtandao wa Bidii habari ndiyo hiyo: Hali si shwari. Kuna hali ya hofu kwa wazazi wenye watoto wao maeneoyale (shuleni) ambao wanatafuta kila namna ya kupata watoto wao nahawapatikani.Red Cross ndo wanawasili sasa hivi. Kuna bomu ambalo linaelekea kulipuka muda wowote kuanzia sasa. Motounaendelea kuwaka tena kwa kasi kubwa zaidi.Kama ulivyosikia Waziri akitangaza, mlio kwenye majengo marefu Darmkae mkao wa kukimbizana likilipuka lile linalohofiwa."

Mwingine kaandika hivi kwenye Bidii:Nipo hapa office za zantel,milipoko hiyo imesababisha watu wote kutoka nje kutona na mtikisiko mkubwa uliotokea karibu mara mbili hivi.Mlipoko huo umesababisha kuvunjika baadhi ya vitu, vitu hivyo zikiwemo laptop mbili za wateja ambao walikuja kupata huduma ya kuunganishwa na mtandao.

Habari zaidi fuatilia hapa...

No comments:

Post a Comment