Wednesday, April 29, 2009

Hali sasa Tulivu-Lukuvi

Wananachi wakiangalia mabaki ya mojawapo ya mabomu yaliyoruka umbali wa km4. Ni moja ya takriban ya mabomu 12 yaliyolipuka na kutua uraiani...

Taarifa zilizotufikia muida huu na kukaririwa na Globu ya Jamii ,Mkuu wa Mkoa wa Dar, William Lukuvi, hali kwa sasa ni shwari na wadau wanaweza kurejea majumbani mwao.
Zaidi ni kwamba, majeruhi wengi wamepelekwa hospitali ya Temeke wengine Muhimbili, inasemekana watu takriban 100 wamejeruhiwa. Aidha, majengo ya shule ya St. Anthony yaliathirika kwani vioo vya madirisha karibu yote yamevunjika, na nyumba kibao zimeharibika.

No comments:

Post a Comment