Sunday, August 07, 2005

Hayawi Hayawi Yamekuwa

Yameshakuwa. Wazee walie tu. kambi ya vijana imepeta katika kinyanganyoro cha viti vya ubunge nchi nzima. Hadi naku;letea habari hizo tayari wazee wengi, wakongwe katika siasa za Tanzania na waliodhani wamerithi viti vya ubunge wameanguka. Miongoni mwa walioangushwa na vijana ni Dk. Laurence Ghama wa Songea Mjini Prof Simon Mbilinyi wa Peramiho, Prof Pius Mbawala wa Namtumbo, Stephen Kazi wa Nyamagama (mwanza mjini), Dk. Hassy Kitine (Makete), George Mlawa (Kalenga), Thomas Nyimbo (Njombe Magharibi), Dk. William Shija (Sengerema), Waziri Daniel Yona (Same Magharibi) na wengine kibao. Sura mpya ni zipi? Nitakupa

1 comment:

Jeff Msangi said...

Inatia moyo sana.Kazi nzuri ndugu yangu.Tafadhali nipatie list ya vijana wapya katika kinyang'anyiro hiki ukiikamilisha.Kazi njema.

Post a Comment