Sunday, April 05, 2009

Swali la Kuokota

Kuokota si kuiba: Swali hili nimeliokota kwenye Bidii@googlegroups.com

Ndugu Zangu,

Nimekuwa najiuliza ni kwa nini waandishi wa habari wa Tanzania ni rahisi sana kuwa “twisted’ kiasi ambacho wako tayari kutetea uovu kwa nguvu zao zote?. Je ni kwa kuwa biashara yao ni ngumu sana kiasi ambacho bila kununuliwa hawata”survive” au ni kwa kuwa taaluma ya Uandishi wa Habari haina “Professional Ethics” zinazoongoza taaluma hiyo?

Je mishahara ya waandishi wa habari ni midogo sana kama ya Polisi wa Usalama barabarani? Singeshaa sana kama wanaotetea uovu huo wangekuwa waandishi wachanga ambao wamesomea kwenye hivi vyuo “disposable”. Cha ajabu ni kwamba wakongwe ndo wamejiingiza kwenye kutetea maovu. Mfano mzuri ni hili suala la Dowans na binamu yake Richmond. Walioko mstari wa mbele kuwatetea waovu hawa waliovuna pesa zetu bila kupanda ni Waandishi wa Habari tena wakongwe!

Je inawezekana kuwa baada ya umri kupitiliza bila wakongwe hawa kuwa na “defined future” wameona bora watoke kupitia Dowans?

Nawakilisha.

No comments:

Post a Comment