Saturday, February 12, 2005

Wakubwa wameondoka, Dodoma imenuna tena

Jana, Ijumaa Mkutano wa 18 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano ya Muungano uliahirishwa. Mheshimiwa sana Spika Msekwa alitoa ruksa kwa Waziri Mkuu Sumaye kuahirisha bunge hadi April. Kuanzia leo, wakubwa wameanza kurejea kwenye mji wao wa joto, Dar. Ingawa misaafa ya hapa kwetu inasema Dodoma ndio mji mkuu wa Tanzania, ukweli ubaki pale pale kuwa makao makuu halisi yapo Dar es Salaam, mji wenye vivutio vya kila aina. Ndio hivyo tena wazee wameondoka. Mashangingi (Landcruiser) nayo yamepungua mjini. Vimebaki vigari gari vilivyochakaachakaa. hakutatokea magari ya gharama kubwa kama hayo kugongana tena kama ilivyokea majuzi, ambapo gari la Waziri Migiro na Mbunge Kasaka yalipobamizana uso kwa uso.
Katika Bunge hili kuma mambo mengi yaliyoleta changamoto, moja kuwa lilikuwa la mabadiliko ya katika ya nchi, ambayo hata hivyo, Kambi ya Upinzani imesema yalikuwa danganya toto. Imepita kwa kura za wabunge wa CCM pekee baada yawake wa upinzani ku-'walk out', isipokuwa wale wabunge wawili wanaobezwa na wenzao kuwa ni mahakama. (walifukuzwa na vyama vyao, mahakama ikawarejesha. Kutokana na uamuzi huo, Sumaye amewabeza kuwa hawajui kanuni za bunge, wamekimbia mjadala badala ya kukaa na kujenga hoja.
Kubwa zaidi, mbali na shughuli za bunge, vyombo vya habari vilitawaliwa na issue ya kukombea urais wa Tanzania. Wiki ijayo, Halmashauri Kuu wa CCM inakutana hapa kupitisha pamoja na mambo mengine, ratiba ya uchukuaji fomu za kuomba kugombea urais kupitia chama hicho hapo Machi. Hapo ndo tutaona kivumbi na jasho, mbio kali kali na chafu, ilimradi kila mtu aingie IKULU ya Chamwino, sorry, ya Mtaa wa Lutuhuli, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment