Friday, February 04, 2005

UTABIRI UMETIMIA:'Makao Makuu yako Dodoma'

YALIYOTABIRWA yameshatimia. Makao Makuu ya nchi sasa yako Dodoma. Waheshimiwa wote, isipokuwa rais na amakamu wake, wamejaa hapa tele kama pishi la mchele. Ukitembea mji mzima wa Dodoma, unakutana tu na magari ya kifahari, ambayo hayapo popote Afrika. Haya ni 'mashangingi' au kwa jina lake halisi Toyota Landcruiser ama GX au VX. Ukiingia baa utakutana na waheshimiwa wale wale.
Kilichowakalisha hapa pamoja na mambo mengine ni kupitisha Mabadiliko ya 14 ya Katiba. Yaani tangi nchi ipate katiba yake ya sasa mwaka 1977, imeshawekwa viraka 14 na wabunge wanasema hoja na maoni yote ya wananchi, waliyojadiliwa na kupitishwa katika waraka namba 1 wa serikali 'white paper' juu ya katiba hayakuzingatiwa yote. Hapa ina maana kwamba katiba yetu itaongezwa viraka vingine zaidi, na unaweza kuikuta katika hali ambayo haijulikani kitambaa kilichotangulia kilikuwa na rangi gani! si maajabu hayo!
Hoja za baadhi ya wabunge achilia mbali wale 'mbumbumbu wa sheria, ni za msingi, lakini hazimo katika katiba ya sasa; na wale wachache 'wenye nchi' hawafikirii hata kidogo kuyaingiza. Tunaendelea kuwa na 'waheshimiwa' hawa hapa Dodoma hadi mwisho wa wiki ijayo.
Tutaelezana yanayojiri.

No comments:

Post a Comment