Saturday, February 26, 2005

Njia ya Ikulu ni nyembamba kama ya Mbinguni

Mbona wanangu mnakanyagana wakati njia ni pana sana? au mnadhani njia hiyo ni nyembamba kama ya mbinguni?
Maswali hayo ndiyo unayoweza kuwauliza wazee wetu wakati huu, hasa ukishuhudia pilikapilika zao za kutaka kwenda Ikulu. wanashikana mashati si utani, Wanariadha wetu katika mbio hizo za Ikulu, wasiojali kuogopwa kama Ukoma (rejea hotuba ya mwalimu Nyerere kwa wanaokimbilia ikulu, 1995), wako katika kasi ya ajabu.
Wengine wanatembelea wajumbe wa NEC, Mkutano Mkuu wa CCM na 'kuwawezesha', wengine wamenunua magazeti na vyombo vingine vya habari. Juzi, mjini Dodoma, gazeti moja jipya la kila wiki, lilichapisha habari katika uk. wa kwanza kuwa, Baraza la Mawaziri la mmoja wa wagombea urais limevuja. Waliomo wakatajwa waziwazi. Tulishangaa, Nakala za gazeti hilo zilikusanywa mtaani kwa gharama zozote ziwazo na kuteketezwa na ama wapambe au mgombea mwenyewe.
yangu macho, natarajia vituko zaidi na ninazidi kuwaona wakichafuana. Mie, Kama Mkapa. Sina Mgombea.

1 comment:

Anonymous said...

Tupe kwa kina zaidi kuhusu gazeti lililovujisha habari na kukusanywa haraka haraka ili lisiwafikie wananchi. Tafadhali.

Post a Comment