Tuesday, April 07, 2009

Tangazo la DECI

Nimesikia tangazo Wapo Radio kutoka kwa uongozi wa DECI kuwa, leo Ofisi zote zimefungwa 'kuadhimisha kumbukumbu ya Karume'; Kesho pia zitafungwa kutoa nafasi kwa wanachama 'wanaopanda na kuvuna fedha' kujumuika katika mkutano wa wanachama wote katika ukumbi wa PTA, Sabasaba. Wasiwasi wangu, wenye mradi watajitokeza hadharani hiyo kesho, au ndo hivyo tena! Lakini, Cheki Hapa wenye mioyo migumu waliendelea kupanda na kuvuna hiyo jana.
Karume Day Njema!

-RSM-

No comments:

Post a Comment