Monday, October 10, 2005

FFU waanza kusababisha ghasia!

Polisi wanaodhaniwa wa kutuliza ghasia wameanza tena kusababisha ghasia visiwani zanzibar. Na Inaarifiwa kuwa watu 18 wamejeruhiwa, kati yao wanane kwa risasi. Soma hapa. Pia wengine kadhaa, wote mashabiki wa chama cha upinzani cha CUF, wametiwa mbaroni. Kama picha hii ya Khalifan Said wa The Guardian inavyoonyesha.

3 comments:

Indya Nkya said...

Hawa nadhani ndio kazi yao. Askari wa kuleta ghasia, si watulizaji hata kidogo. Hii hali ya Zanzibar isipoangaliwa kwa jicho na mtazamo pevu tutajikuta pabaya!!

Ndesanjo Macha said...

Kweli kabisa. HIlo jina la "askari wa kuzuia ghasia" linapotosha. Askari hawa wakifika mahali penye usalama lazima ghasia izuke, kwanini?
Fela Kuti anaimba kwenye wimbo mmoja juu yao anasema: "blood, sorrow, and tears is their regular trademark."

mloyi said...

ndesanjo na indya wamesema, Hiyo ndiyo kazi yao, wanapata kula yao kwa kazi hiyo, vyeo vinapanda kwa hilo, uwepo na udume wao pia unaelezeka kwa hilo.
tusiwalaumu sana, labda mafunzo yao yana waharibu, hapana yanawajenga, fikra zao wawe hivyo kama wale wenzao na rafiki zao wakubwa, mbwa wa polisi.
juzi juzi kulikuwa na makala ya wapiganisha kuku kwenye Tv,nadhani pulse au Itv, iangalie uone wanavyofundisha hao kuku.

Post a Comment